pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Wapalestina waanzisha mashambulizi makali katika vitongoji vya Israel

Wapalestina waanzisha wimbi jipya la mashambulizi
Wanamapambano wa Palestina wameanzisha wimbi jipya la mashambulizi ya makombora katika vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kujibu mashambulizi ya kikatili yanayofanywa na Israel katika Ukanda wa Ghaza. Leo Jumapili wanamapambano wa Palestina wameshambulia vitongoji mbalimbali vya walowezi wa Kizayuni kama vile Sdot, Negev, Nahal Oz, Alumim na Eshkol. Ving'ora vya tahadhari vimesikika pia leo katika vitongoji vya Hof Ashkelon, Eshkol na Sha'ar HaNegev. Wakati huo huo jeshi la utawala wa Kizayuni limekiri kuwa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina ina nguvu ambazo hazikutarajiwa na Wazayuni. Televisheni ya Nasim imenukuu duru za Kiarabu zikisema kuwa, jeshi la utawala wa Kizayuni leo limesema kwamba, wanamapambano wa Palestina wamefanikiwa kupenya na kuingia katika kitongoji cha walowezi wa Kizayuni na kambi ya kijeshi ya Zakim ya Israel. Israel umewataka walowezi wa Kizayuni wakimbilie kwenye mahandaki hadi watakapopewa taarifa zaidi. Katika upande mwingine Hamas imemlaumu Ban Ki moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa msimamo dhaifu sana aliouchukua kuhusu jinai za Wazayuni huko Ghaza na kusema kuwa, Ban ni mshirika wa jinai za Israel. Televisheni ya "Filastin al Yawm" imemnukuu msemaji wa Hamas, Sami Abu Zuhri akisema hayo leo na kuongeza kuwa, utawala wa Kizayuni unashambulia hata shule na vituo vya Umoja wa Mataifa huko Ghaza, lakini Ban Ki moon ameshindwa kuchukua hatua yoyote ya maana.

0 comments:

Post a Comment