pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

watoto waliouawa katika vita vya Ghaza wafikia 350, Israel yabomboa misikiti na mahospitali leo huko Ghaza

Israel imeua watoto 350 katika vita vya Ghaza
Jeshi la utawala haramu wa Israel limewaua watoto zaidi ya 350 hadi sasa katika hujuma yake inayoendelea katika Ukanda wa Ghaza.
Kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Palestina, watoto hao wameuawa tokea Israel ianzishe hujuma yake ya kinyama dhidi ya Ghaza Julai 8. Taarifa hiyo imeongeza kuwa watoto pia ni thuluthi moja ya zaidi ya Wapalestina 9,000 waliojeruhiwa huko Ghaza.
Hayo yanaripotiwa katika hali ambayo utawala haramu wa Israel ungali unaendeleza hujuma yake za kinyama dhidi ya Ukanda wa Ghaza. Hadi sasa zaidi ya Wapalestina 1,700 wameuawa shahidi katika hujuma ya kikatili ya Israel dhidi ya eneo hilo ambalo pia liko chini ya mzingiro. Kwa ujumla ni kuwa, asilimia 80 ya waliouawa katika hujuma ya Israel huko Ghaza ni raia wakiwemo wanawake 200 na wafanyakazi wa sekta ya afya.
Wakati huo huo msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, Sami Abu Zuhri ameituhumu Israel kwa kukiuka mapatano ya usitishaji vita yaliyofikiwa Ijumaa kwa upatanishi wa Umoja wa Mataifa. Amesema Israel ilijaribu kutumia mapatano hayo kujipenyeza zaidi Ghaza na kwamba wanaharakati wa Palestina walikabiliana na hujuma hiyo kwa lengo la kujihami. Msemaji huyo wa Hamas amesema hatua ya Israel ya kuwashambulia raia na hasa wanawake na watoto ni ishara kuwa utawala huo wa Kizayuni umeshindwa vitani.

MISKITI NA MAHOSPITALI


Israel yabomboa misikiti na mahospitali Ghaza
Utawala wa Kizayuni wa Israel haujatosheka kwa kuwaua kwa umati wanawake na watoto wa Ghaza bali pia umeharibu kwa mabomu idadi kubwa ya misikiti na mahospitali katika ardhi hiyo ya Wapalestina.
Kanali ya Televisheni ya Al Mayadeen imeripoti kuwa katika hujuma ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza mahospitali na vituo vya afya 44 vimeharibiwa kabisa. Hivi sasa aghalabu ya Wapalestina waliojeruihiwa katika vita vya Ghaza hawana sehemu za kupata matibabu.  Mbali na kubomoa mahospitali, jeshi la Kizayuni pia limeharibu kabisa misikiti 41 katika Ukanda wa Ghaza. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, jeshi la utawala haramu wa Israel limeshambulia na kubomoa misikiti hiyo ambayo ilikuwa sehemu ya hifadhi ya Wapalestina ambao nyumba  zao zimeharibiwa kwa mabomu.
Wakati huo huo katika kujibu jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel, Brigedi ya Izzuddin Qassam tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imevurumisha makombora katika miji inayokaliwa kwa mabavu na Wazayuni. Aidha wanamapambano ya Palestina wamefanikiwa kuwaangamiza wanajeshi wasipungua 131 wa utawala wa Kizayuni katika vita vya Ghaza.

0 comments:

Post a Comment