pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Obama: Iran imetekeleza ahadi zake za nyuklia

Obama: Iran imetekeleza ahadi zake za nyuklia
Rais Barack Obama wa Marekani amesisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetekeleza kikamilifu ahadi zake kwenye makubaliano ya nyuklia na kuongeza kuwa, ataupigia kura ya veto mpango wowote utakaowasilishwa kwenye Baraza la Kongresi la nchi hiyo wenye shabaha ya kuvuruga mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1. Akizungumza na kanali ya televisheni ya CNN, Rais Obama ameongeza kuwa, Iran imetekeleza kikamilifu ahadi ilizozitoa kwenye makubaliano ya muda ya nyuklia na kusisitiza kwamba pande hizo mbili zina fursa ya kufikia makubaliano ya mwisho. Rais wa Marekani ameelezea changamoto anazoweza kukabiliana na mrengo wa Republican kwenye kongresi  kuhusiana na miradi ya nyuklia ya Iran inayaotekelezwa kwa malengo ya amani na kusisitiza kwamba, jambo lililo na umuhimu ni kufikiwa makubaliano ya mwisho. Kuhusiana na mpango wa John Boehner   Spika wa Kongresi ya Marekani  wa kutaka kumualika Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa Israel na ahutubie kwenye kongresi, Rais Obama amebainisha kwamba hatakutana na Netanyahu kwenye safari yake ya Washington. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mrengo wa Republican wenye viti vingi kwenye kongresi, unafanya njama za kuvuruga mwenendeo wa mazungumzo ya nyuklia kutokana na mashinikizo ya Lobi ya Wazayuni. Mrengohuo pia unataka kupitisha vikwazo vipya dhidi ya Iran, suala ambalo limekabiliwa na radiamali kali ya Obama na viongozi wengine wa White House.

0 comments:

Post a Comment