pagead2.googlesyndication.com pagead2.googlesyndication.com

Waliofungwa kesi ya EPA waachiwa

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imewaachia huru wafanyabiashara watatu, wakiwemo mume na mke, waliokuwa wamehukumiwa kifungo cha miaka 13 na miezi sita jela kwa sababu ya wizi wa Sh bilioni 1.1 katika Akaunti ya Madeni ya Nje ya (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Walioachiwa huru ni mume Manase Makale na mkewe Edda Makale, na mfanyabiashara mwingine Bahati Mahenge.bWashitakiwa hao waliachiwa mwisho wa wiki iliyopita baada ya Jaji Augustine Shangwa kukubali rufaa iliyowasilishwa na
wafanyabiashara hao kupinga hukumu
iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwaka jana.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji Shangwa alisema anawaachia huru wafanyabiashara hao kwa kuwa upande wa Jamhuri ulishindwa kabisa
kuthibitisha mashitaka dhidi yao Aliamuru wafanyabiashara hao waachiwe huru mara moja na kutengua amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyowataka warejeshe fedha hizo mara baada ya kutumikia kifungo.
Katika rufaa, wafanyabiashara walikuwa wakipinga hukumu iliyotolewa na jopo la mahakimu Sekela Mushi, Sam Rumanyika na Lameck Mlacha, wakidai kuwa kulikuwepo na upungufu mkubwa wa kisheria nankihoja katika kuwatia hatiani. Katika hukumu iliyotolewa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mahenge alitakiwa kutumikia kifungo cha miaka saba jela, Makale kifungo cha miaka mitano jela na mkewe Edda kifungo cha mwaka mmoja na nusu.
Aidha, mahakama iliamuru baada ya
kutumikia adhabu hiyo, Mahenge na Makale warejeshe kiasi cha Sh bilioni 1.18 walichodaiwa kukiiba katika akaunti ya EPA. Washitakiwa walikuwa wanakabiliwa na mashitaka ya kula njama ya kutenda kosa, kughushi nyaraka mbalimbali na kuziwasilisha sehemu husika na kuiba fedha hizo.
Katika kesi hiyo, wafanyabiashara hao
walikuwa wameshitakiwa na wenzao Davis Kamungu na Godfrey Mushi ambao waliachiwa huru katika Mahakama ya Kisutu kwa kuwa upande wa Jamhuri ulishindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao bila kuacha shaka.

0 comments:

Post a Comment